https://www.revenuecpmgate.com/wyyr1iikfh?key=e991cdff29305dd0cd3e6cdadd05a86b
https://www.videosprofitnetwork.com/watch.xml?key=a678b2cd8354f76d0fd632f604db00b4
https://www.videosprofitnetwork.com/watch.xml?key=a678b2cd8354f76d0fd632f604db00b4

THE STORY BOOK

https://www.revenuecpmgate.com/wyyr1iikfh?key=e991cdff29305dd0cd3e6cdadd05a86b

Thursday, 10 October 2019

11:00 PM - 1

Simulizi : 11: 00 pm
Sehemu Ya Kwanza (1)

Mziki laini kutoka kwa muimbaji john macnair uitwao we are together ulizidi kukonga nyoyo za wageni waalikwa waliofika kuhudhulia hafla hii kubwa kufanyika nchini uingeleza

viongozi kutoka mataifa mbalimabali hasa hasa africa na nchi za kutoka bara la asia walifika kuhudhuliua sherehe hii kubwa iliyoandaliwa na malkia georgia

kila mgeni mualikwa aliyekuwa kwenye ukumbi ule mkubwa alikuwa na furaha ya aina yake glass za vinywaji zikagongeshwa huku viongozi waliokaa vikundi vikundi walikuwa wakiteta hili na lile

saa nne na dakika robaini na tano malkia georgia wa uingeleza akasimama mbele ya ukumbi sura yake ikiwa imevaa tabasamu kubwa sana

ulinzi uliokuwa mahala pale ulimfanya malkia huyu ajiamini kupita kiasi,vioo visivyopitisha risasi vilimpa kibuli kikubwa ukiachilia mbali walinzi waliokuwa mahala hapa

mmh mmh" aliguna kutoa vumbi kooni kisha akapiga funda mbili za wine ya queen elizabeth akaludisha tabasamu usoni mwake kisha akaanza kuwaangalia viongozi waliofika mahala pale kwa macho ya tuo alipomaliza akakishika kipaza sauti na kukigonga kwa juu sauti ikasikika

akachukua kipaza kila na kuanza kuongelea maswala ambayo yalipelekea kuwepo kwa kikao kile

kikao chetu kinahusu mladi mpya wa uchimbaji madini na mafuta'aliongea malkia kisha akanyamaza kidogo viongozi wote walikuwa mahala pale walikuwa kimya wakimsikiliza

...
Bunduki maalufu kwa kupiga masafa marefu (FK) (festikovik kesktivicky) iliyotengenezwa nchini urusi na kutumika kwenye vita ya pili ya dunia ilikuwa imekaa tayari juu ya jingo kubwa la kibiashara la home sweet

mlenganji aliyekuwa akitumia bastora ile alikuwa makini akifuatilia kila kilichokuwa kinaendelea ndani ya ukumbi ule alikuwa akijua kila kitu kuhusu ulinzi uliokuwa mahala pale ukiachilia mbali kile kioo kisichopitisha risasi

sasa zilibaki dakika tano kufika saa tano kamili saa kubwa ya clock tower iliendelea kumaliza dakika hizo

malkia georgia alizidi kuhutubia mkutano wake ambao mada kubwa ni kuanzisha kiwanda cha pamoja ambacho kitapelekea kila nchi kunufaika na madini yao

kampuni ya word mining ndio iliyokuwa ikizungumziwa kila wakati huu ulikuwa mladi mkubwa ambao haukuwai kutokea sasa ndio ulikuwa ukipangwa kufunguliwa

viongozi kutoka nchi ya malekani hawakuliafiki hili swala moja kwa moja wakamtuma mtu wao kuja kulifanya hili tukio liwe ndoto shabaha iliyowekwa ni kumuua malkia georgia na rais kutoka nchi za east africa nchi ya Tanzania ambapo kitovu cha kuzalisha madini mengi barani africa na dunia kiujumla

nchi ya urusi na japani ziliungana na malekani kupinga hili swala huku ujerumani nalo likizidi kutia nguvu juu ya mpango huu mkubwa usitokee kwani nchi zao zitapitwa kiuchumi na nchi nyingi za africa zitafanikiwa kiuchumi

hapo kikaundwa kikundi cha siri kutoka katika hizi nchi nne ,kikundi cha kumuangamiza malkia na raisi wa tanzani hawakuishia hapo wakafanya mkutano wa siri nchini sudan kwenye jumba kubwa la king suddi tajiri aliyeheshimika kwa kuuza mafuta duniani huku wakimshirikisha bwana alex ndaro makamu wa raisi wa Tanzania kuingia kwenye mkakati huu pia waziri mkuu wa uingereza bwana thomson naye alikuwapo katika mpango huu mkubwa

sekunde zilikatika hatimae zikabaki sekunde tano kuaga saa nne kuingia saa tano kamili mlengaji yule alikaa makini kutekeleza kile kilichopangwa

akakiweka kidoer chake sehemu ya kufyatulia risasi kisha akavuta pumzi kwa kasi na kuhifadhi kifuani mwake akabinya jicho lake moja kisha lingine likatua kwenye lenzi ya bastora ile

zile sekunde tano zikaisha sekunde zilizobeba uhai wa malkia huyu mlengaji yule aliyeonekana yupo makini na kazi yake akaachia risasi mbili mfululizo moja ilipiga kwenye kioo na kuweka ufa nyingine ikapasua kii na kupita kisha ikatua kwenye kichwa cha malkia huyu damu zikaluka huku na kule ubongo ukatawanyika na kuchafua kuta za ukumbi ule

tafrani ikazuka ndani ya ukumbi ule kila mtu alikimbilia mahala ambapo aliona anaweza kuinusuru roho yake

walinzi waliokuwapale wakaanza kuangaza huku na kule wakitafuta mahala ambapo risasi zile zilitokea bila mafanikio

yule mlengaji alivyofanikiwa kumdungua malkia akakusanya siraha zake na kuziweka kwenye mfuko mmoja kisha akachukua bomu la dakika na kuliweka kwenye ule mfuko alivyomaliza akavua nguo zake za kazi na kuziweka kwenye lile begi sasa akabaki akiwa na suti zilizomkaa vizuri

akauendea mlango uliokuwa juu ya ghorofa ile akaufungua kisha akazama kwenye lift iliyokuwa pembeni yake akapanda na kushuka katika ghorofa ya kumi na mbili chini ambapo kulikuwa na casino

baada ya kutoka kwenye lift ile akaelekea counter na kuagiza wine kisha akaanza kuikata taratibu huku akiwa kimya kama anafikili jambo

dakika tano baadaye mlipuko mkubwa ukatokea juu ya ghorofa ile tafrani ikatokea kwenye casino ile watu walikimbia huku na kule kunusuru maisha yao

akiwa bado yupo counter ving'ora vya magari ya polisi vikaanza kusikika vikija kwa kasi


Ving'ola vilizidi kusikika vikija mahala pale ,watu waliokuwa ndani ya casino ile wakaanza kukimbia huku na kule

magari maalumu ya wagonjwa (ambulance) na maengine ya kuzima moto yalianza kuja kwa kasi mahala pale

baada ya yule muuaji kuona mapolisi wanakalibia akapeleka mkono wake mfukoni na kutoa kikopo kidogo cheupe akafungua kizibo chake na kumimina vidonge vitatu mkononi mwake kisha akavimeza

baada ya kunywa vile vidonge mwili wake ukaanza kuishiwa nguvu kwa kasi kubwa na dakika chache baadaye akadondoka chini

vikundi vya uokoaji viliingia ndani ya casino ile kuokoa kama kuna mtu aliyepata tatizo lolote huku wengine wakipanda rift kuelekea ghorofa ya juu wakishirikiana na wataalam wa mambo ya milipuko

wale watoa huduma ya kwanza walioingia club walimuona mtu akiwa amelala kwenye meza wakamchunguza kwa mashine zao maalum wakatambua hakuwa na tatizo lolote zaidi ya kuzidiwa na ulevi askali wa usalama wa raia wakamchukua na kumuweka kwenye gari kisha wakampeleka kituoni kutumikia kifungo cha masaa kadhaa

Taarifa za kuuwawa kwa malkia wa uingereza zilizidi kuenea kwa kasi kwene pembe za duniani

kitendo cha kudunguliwa kwa malkia yule kilitasfili kama kitendo cha kigaidi ambacho hakikuwai kutokea katika Taifa hilo la uingeleza

vituo vikubwa kama sky news ,aljazeera na bbc word vilizidi kutangaza na kulaani tukio hili kubwa makundi makubwa makubwa ya kigaidi yalishutumiwa juu ya swala hili la kuuwawa kwa malkia georgia wa uingeleza

bendera za nchi hiyo zilishushwa nusu mlingpti kuomebeleza msiba huu mkubwa uliogubika huzuni kwenye mioyo ya waingeleza wengi

watu wenye asili ya kiarabu walianza kukamatwa na kuhojiwa huku viwanja vyote vikubwa vya ndege vikisitishwa kufanya kazi

07:12 am .mlango wa kituo cha polisi cha crystal ulifunguliwa kisha mtu aliyekuwa mule ndani akatoka akakabidhiwa vitu alivyokuja navyo kisha akasaini na kuondoka mahala pale

safari yake iliishia kwenye kituo cha mabasi yaendayo kwa kasi akakaa kwa mda mahala pale hadi gari kubwa jeusi lilipokuja kusimama mbele yake akasimama na kuingia ndani ya gari ile kisha akatokomea nje ya mji

umefanya kazi nzuri sana naamini mipango yetu itakwenda vizuri na kama itatimia vile tulivyopanga bhasi utakuwa mtu mkubwa sana nchini kwenu"aliongea sir thomson waziri mkuu wa uingeleza huku akiwaacha wenzie wakimuangalia kijana wao kwa sura ya tabasamu

mkutano wao wa siri uliendelea kufanyika nje ya jiji hili kubwa la london kazi iliyobakia ni kumuua raisi wa tanzania ili mladi ule ufe

hapo ikapangwa mipango mingi sana huku taarifa kali na za siri zikitoka kwa makamu wa raisi wa tanzania bwana alex ndaro

mazishi yanafanyika baada ya wiki mbili katika makabuli ya kifalme yaliyokuwa katika lile jengo kubwa hivyo unatakiwa kuificha labda kwenye gari au kwenye makaburi mengine yaliyokuwa mahala pale au kwenye ghorofa lenye mnara wa saa"aliongea sir thomson huku akimuangalia kijana wao wakazi

msafara mlefu uliotoka katika kanisa kubwa katoliki lililopo hapo london ulianza kuelekea kwenye makaburi ya kifalme yaliyokuwa kwenye jengo hilo kubwa ,mamia ya waombolezaji walikuwa mahala hapo huku sura zao zikifunikwa kwa miwani mieusi ,wamama walivaa nguo nyeusi na wazee wakavaa suti nyeusi vituo vikubwa vya cctv,bbc,cnn,aljazeera vilishindana kuchukua taarifa muhimu mahala pale

ndege za usalama zilikuwa angani zikidumisha usalama huku magari ya huduma ya kwanza nayo yalikuwa mahala pale

baada ya mwili wa malkia kufikishwa mahala pale

wanajeshi wenye nyota kadhaa waliovalia nguo nyeupe zenye mikanda mieusi na kofia nyeusi wapatao nane walilibeba jeneza la malkia lililovalishwa bendera ya uingereza kisha wakalipeleka hadi sehemu yake maalum padre akausalia mwili kisha ukafikia muda wa kuaga

viongozi mbali mbali wakaanza kuuaga mwili wa malikia wengi wao walikuwa na vitambaa vilivyojaa machozi ya hudhuni hasa huyu raisi wa Tanzania hakutaka kuamini kabisa kama malkia amefaliki dunia alijikuta akiwalaani kila waliotelekeza jambo hili la kigaidi

mlengaji wa masafa malefu akiwa bastor yake nyingine mfano wa ile ya kwanza alikaa makini juu ya paa la uwanja mkubwa wa mpira nchini uingereza

zilikuwa kilometa zipatazo kumi na moja kutoka pale alipokuwapo na sehemu ya mazishi hii bunduki aliyokuwa nayo leo haikuwa ya kawaida ilikuwa na uwezo wa kurusha risasi masafa malefu sana

upepo uliokuwa ukivuma haukuweza kuzuia shabaha ya mlengaji huyu aliyeonekana kubobea kwa kazi hii kwani baada ya Raisi wa Tanzania kulifikia jeneza la malkia risasi tatu za nguvu zilipenya kwenye mwili wa bwana huyu moja ilipenye kifuani nyingine tumboni na nyingine ikapiga kichwani na kutawanya ubongo na damu

tafrani ikatokea mahala pale camera zilinasa tukio zima la kupigwa risasi hadi umauti wake gari za huduma ya kwnza zilifika mahala pale ila tayari alishakufa mwili wake ukielea juu ya dimbwi la damu nzito

Polisi na maofisa usalama walizidi kuchanganyikiwa juu ya huyu mtu anayepiga masafa marefu ,vikosi maalumu vya kupambana na ugaidi viliingia kazini kufanya kazi yao kazi ya kumtafuta huyu bwana anaye endeleza mauaji kwa viongozi wakubwa

baada ya yule muuaji kufanikiwa kumuua raisi wa Tanzania akachukua ile bunduki yake na kuiweka kwenye mfuko mdogo kisha akavua nguo alizovaa na kuziweka kwenye ule mfuko kisha akatega tena lile bomu lake la dakika,baada ya kumalizia kutega bomu akaondoka huku akipiga mahesabu dakika kadhaa baadaye mlipuko mkubwa utatokea

mwendo wake wa kasi ulitosha kabisa kumfikisha nje ya uwanja ule mkubwa katika nchi ya uingereza akaendea tax iliyosimama pembeni ya barabara kisha akazama na kutokomea mahala pale

vyombo vingi vya habari vililipoti juu ya tukio la kuuwawa rais john mambo wa Tanzania huzuni iliyoikumba England sasa ikaamia Tanzania raia wengi wa nchi hiyo walibaki na majonzi makuu juu ya raisi wao mpendwa kuuwawa kwani alijitoa sana kwenye jami kushinda maraisi wenzie waliopita akatokea kukubalika kupendwa ila leo hii amefariki dunia kwa kudunguliwa risasi tatu ambazo zilitafsiliwa kama miaka yake ya utawala tangu aliposhinda kiti cha uraisi

sasa zilipita sikutatu tangu kifo cha raisi wa tanzania kitokee nchi ya england ikishirikiana na Tanzania ziliamua kuungana na kuanza kulitafutia ufumbuzi swala hili

kwa serikali ya Tanzania alichaguliwa TSA lilyan Dismas huyu alikuwa mpelelezi imara hata akafanikiwa kuwakamata watu wanaojihusisha na mauaji ya albino kwa upande wa uingeleza wakamchagua bwana smith

timu hii ya wapelelezi wawili ikaingia kazini huku wakianza kuchunguza kuanzia kule casino wakaagiza walinzi wote wa siku hiyo wapelekwe kwenye chumba maalum kwa ajli ya mahojiano kisha kumbukumbu zote zilizochukuliwa na camera kwa siku hiyo ziletwe

baada ya kumaliza mahojiano na walinzi wale pamoja na wahudumu wakachukua cd iliyorekodiwa matukio yote ya siku ile kisha wakaanza kuangalia

waliona watu wengi wakiingia ila macho yao yakatua kwa kijana mmoja mweusi ambaye aliingia akiwa na briefcase mkoni mwake

walimfatilia hadi anaingia kwenye lift kisha akapanda na kwenda hadi ghorofa ya mwisho na baada ya dakika chache walimuona mtu yuleyule akiwa anashuka bila briefcase huku akiwa amebadili nguo na kuvaa suti ,wakaanza kumtilia shaka bwana yule walichokifanya wakaomba na kumbukumbu za video zilizochukuliwa na camera kwenye uwanja wa mpira ajabu wakamuona tena yuile kijana akiwa anaingia huku mkononi mwake akijifanya anapigapiga picha baada ya hapo wakamshuhudia akielekea upande ambao mlipuko ule ulitokea hapop wakajihakikishia kuwa huyu ndiye muuaji mwenyewe

baada ya kujihakikishia wakatoa taarifa kwenye idara zao husika picha zikaanza kusambazwa kwenye kila nchi na hatimae zikamfikia bwana Thomson

kijua cha saa saba kilikuwa kinachoma kwa stairi ya aina yake katika kitongoji kidogo cha bunley nchini england migahawa mingi ilijaa watu kwa ajili ya kujipatia chakula cha mchana

katika mgahawa mmoja ulikuwa kwenye mtaa wa st anthony zilisimama gari ne za kifahali kisha watu wanne kutoka kwenye magari yale tofauti wakashuka na kuelekea kwenye mgahawa uliokuwa pembeni yao kila mmoja alionekana na wasiwasi sana juu jambo fulani ambalo linaweza kuwaweka sehemu mbaya pale tu litakapobainika

kama ilivyowaambiaa huyu mtu anatakiwa kuuwawa mala moja"aliongea sir Thomson huku akiwaangalia wenzie kwa macho ya tuo

lazima tummalize akikamatwa awezi akatuacha na sisi atatuweka matatani "aliongea captain ji park huku akionekana na hofu sana

sir edward waziri wa biashara nchini malekani na bwana stuart waziri wa madini nchini ujerumani walikuwa kimya wakiwasikiliza wenzao na baada ya kujadili sana uamuzi ukapitishwa wa kuuwawa kwa yule kijana waliyemtuma kufanya mauaji

ndege aina ya british airline ilibuluza gurudumu zake kwenye uwanja mkubwa wa ndege nchini malekani wa bwana john F kenned ,dakika chache baadaye abilia wakaanza kushuka akiwepo na yule muuaji

akauendea mlango wa watu wanaowasiri kisha akatoka na kuelekea kwenye tax iliyokuwa nje ya uwanja ule akapanda na kuelekea kwenye hotel ya Px iliyopo kwenye jiji la newyork city

ilikuwa imetimu saa tano usiku akawasha kompyuta yake mpakato na kuanza kuangalia hili na lile mara kikaingia kile alichokuwa anakisubilia akaachia tabasamu hasa pale alipoona msg ya email iliyotoka kwa mke wake akaifungua na kuanza kuchat na mke wake huku akijulia hali watoto wake wawili wakike

akiwa anaendelea kuchat mala mlango wake ukagongwa akaenda na kuchungulia kwenye kitobo kilichokuwa pale mlagoni

shiit"alijisemea baada ya kuona maaskali waliovalia nguo za swat wakiwa mlangoni mwake akatambua mabosi wake wamemuuza hasira zikampanda

akiwa hajui nini afanye mala kitasa cha mlango wake kikanyongwa kwa chini kisha funguo inayoweza kufungua milango yote ikaanza kupenyeshwa

akapiga hatua hadi dirishani ili aluke lakini akasita umbali wa ghorofa sita ukampa hofu

Polisi walizidi kugonga ule mlango kwa kasi ya ajabu na dakika chache baadaye kimya kikachukua nafasi yake

polisi kutoka kitengo maalumu cha kuzuia ugaidi Fbi walisimama imala nyuma ya mlango ule ambao gaidi alikuwa ndani id yake ilionesha jina lake ni Eric rwoma butimbwa

kila polisi alishika mtutu wake imala ili kuanza mashambulizi ,ndege mbili kutoka vitengo viwili tofauti vya ulinzi nchini malekani NYPD na FBI zilikuwa zikilandalanda kwenye hotel ile huku taa zao kubwa zikimulika chumba ambacho eric alikuwapo

baada ya kuona polisi wamejaa kila mahala eric akaelekea kwenye bafu la chumba kile kisha akafungua maji na kuchukua kitaulo kidogo akakilowesha na maji kisha akakifunga chini ya pua yake baada ya hapo akafungulia maji ya bafuni hadi mwisho kisha akaiwasha na tv akafungulia sauti hadi mwisho baada ya hapo akapanda kwenye kabati lililokuwa pembeni kwenye ukuta kisha akaanza kupapasa sehemu iliyokuwa wazi na dakika chache baadaye akaipata ,hakutaka kuchelewa akapanda juu ya dari kisha akachukua bomu la kutega kwa sekunde na kulidondosha kwenye kile chumba kisha yeye akaanza kusota kwenye (emergence way) zilizokuwa juu ya dari lile

baada ya polisi wale kuona hamna dalili ya mtu kutoka wakachukua gesi ya kukatia vyuma kisha wakaanza kukata kitasa kile hadi kikaachia kisha wakachukua bomu la machozi wakalitupa ndani ya chumba kile na wao wakavaa mask kisha wakaanza kujitoma ndani ya chumba kile

puuu"ulisikika mlipuko mkubwa kisha kishindo cha watu kudondoka chini kikasikika huku ukuta chumba kile alichokuwa eric ukiwa umesambaratika na kubaki wazi kabisa

mlipuko ule wa bomu ulipelekea askali kadhaa walioingia ndani ya chumba kile kufa papo hapo huku waliobaki nje wakiwa wamejeruhiwa vibaya mno

kitengo cha kuokoa wagonjwa kilikuwa mahala pale na baada ya mlipuko ule wakaanza kazi mala moja ya kuondoa majeruhi na polisi waliofaliki

hasira zilizidi kuwakaba kooni askali wale sasa wakabadili mbinu wakaja na mbwa ambao walikuwa na mafunzo maalumu juu ya milipuko

wakati bomu lile linalipuka eric alikuwa ameshafika chumba cha nane mbele mlipuko ule mkubwa ulimlusha hadi kwenye chumba cha mbele yake

bahati nzuri chumba kile hakikuwa na watu , akajinyanyua mahala pale alipokuwa amedondokea kisha akauendea mlango akaufungua kidogo na kutoa kichwa chake nje macho yake yakatua kwa askali mmoja aliyekuwa amesimama kwenye kordo moja iliyokuwa ikielekea kwenye chumba chake

moshi mkali ulizidi kutanda kwenye kordo zile hivyo eric akajitoa kwenye kile chumba na kumvaa askali yule aliyekuwa amevaa mask usoni akamkaba na kumnyonga kisha akamuingiza kwenye kile chumba na dakika chache baadaye akavaa nguo zake na kumbeba mgongoni mwake na kuanza kutoka naye nje

akiwa anashuka kwenye ngazi za ghorofa ile alikutana na maaskali kadhaa wakiwa wanapanda ngazi kuelekea kwenye chumba kile alichokuwapo
akaanza kushuka kwa haraka haraka na alipofika nje akaliendea gari la wagonjwa kisha akamuweka yule bwana na yeye akaelekea mbele akaliwasha gari na kutimka mahala pale

safari yake ilikuwa ni kutoka nje ya new york na kwa usiku ule barabara zilikuwa hazina magari mengi hivyo akaendesha gari kwa kasi hadi kwenye daraja la brooklyn alipofika mahala pale akaliendesha gari kwa spidi kuelekea kwenye kingo za daraja lile kisha yeye akaruka lile gari likaenda kugonga zile kingo na kuruka hadi baharini huku yeye akajirusha kwa upande wa barabarani

mlipuko mkubwa ukasikika kwani gari lile lilienda kutua juu ya boti lililokuwa likiendesha shughuli za uvuvi usiku huo

06:28 am polisi wa new york na baadhi ya vitengo vingine vya usalama wakafika kwenye eneo lile la mlipuko wakaanza kulivuta gari lile huku uchunguzi ukizidi kushika kasi

barabara zote za kutoka kwenye mipaka ya jiji hilo kubwa ikafungwa huku ulinzi ukizidi kuimalishwa ndani ya jiji hilo kubwa

siku tano baadaye luninga nchini malekani na duniani kwa ujumla zilikuwa zikirusha habari ya kufa kwa gaidi yule aliyemuua queen georgia na raisi wa tanzania furaha zikapamba mioyo ya watu wengi duniani

taarifa za kuuwawa kwa gaidi yule ilikuwa faraja kwa watanzania na wana england kwa ujumla

.......
miezi mitano baadaye Ndege kubwa kutoka kwenye shilika la ndege la malekani klm iliburuza magurudumu yake kwenye uwanja wa taifa wa MWALIMU JURIUS NYERERE

kila abilia aliyeshuka kwenye ndege ile alionekana na furaha sana ila tofauti ilikuwa kwa huy abilia wa mwisho hakuonekana na furaha wala huzuni yeye alikuwa katikati ya yote

baada ya kushuka kwenye ndege ile akauendea mlango wa wanao wasili akaweka begi lake sehemu ya ukaguzi kisha na baada ya taratibu za ukaguzi kukamilika akachukuwa begi lake na kuonoka pale airpolt huku sura yake ikianza kuweka mikunjo punde tu alipoikanyaga ardhi ya Tanzania

karibu tena Tanzania na kabla sijasahau utaanza lini kazi yako"alijisemea kimoyomoyo bwana yule mda huo akiwa kwenye basi linaloelekea mkoni morogoro


Kelele za wapiga debe katika stand ya msamvu iliyopo morogoro ndizo zilizo muamsha eric katika usingizi mzito uliompitia

akajinyanyua kiuvivu kwenye kiti alichokuwapo kisha akashuka kwenye lile gari akaendea taks iliyokuwapo mahala pale na kupanda kisha akatoa maelekezo sehemu ya kupelekwa

akiwa anaangaza angaza huku na kule kwenye ile taks macho yake yakatua kwenye gazeti lililokuwa mbele yake akalichukua na kuanza kulisoma taratibu

kurasa zote alizipita bila kubabaika ila hii kurasa ya tisa ilimpa kibabaishi kichwa cha habari cha gazeti hili kilimpa simanzi moyoni mwake

FAMILIA YA GAIDI YAJIANGAMIZA

kichwa hiki cha habari kilimchanganya zaidi eric bila kupoteza mda akaanza kusima taarifa ile huku moypo wake ukimuenda mbio sana

boss tumeshafika"aliongea dereva wa taks ile huku akigeuka nyuma akimaanisha kupewa ujira wake

baada ya eric kumpatia ujira wake dereva yule akashuka kwenye gari ile lakini akashangazwa na hali ilyokuwapo kwake magali yalikuwa mengi sana huku maturubai yakionesha dhairi kuna tukio

akiwa ameduwaa ajui nini cha kufanya mala akamuona mtu ambaye alikuwa akimfahamu alikuwa askali mwenzie haraka haraka akajitoa mahala pale na kwenda kujificha nyuma ya mti uliokuwa karibu na nyumba yake

kiza kilichoanza kuteka dunia kilitosha kabisa kumficha eric

mimi siamini kama yule mama ameiua familia yake na yeye kujiua"alisikika mama mmoja akiongea kwenye hiki kikao cha watu watatu

hata mimi nashangaa yani mama uliyeshika uchungu unaweza ukadiliki kushika kisu na kuanza kuwacharanga wanao vibaya namna ile"alidakia mama wapili

hapa kutakuwa kuna kitu hata mimi siamini"alidakia mama wa tatu na ukimya ukapita

wakati wale wa mama wanabishana juu ya yale mauaji eric alikuwa akiwasikiliza hasira zikampanda maradufu ila hakutaka kufanya lolote kwa mda huo alichokifanya ni kurudi stand na kudandia maroli yanayoenda mwanza bahati ilikuwa kwake alifanikiwa kupata roli

saa saba mchana lori lile lilifika jijini mwanza eric akashuka na kuwashukuru mabwana wale hakutaka kuendelea kukaa tena katika hili jii alichokifanya ni kwenda kamanga ferry hapo akapanda mery ndogo ya mv krelias ambayo mass matatu baadaye akawa amewasiri kwenye kisiwa cha ukerewe

safari yake haikuishia hapa akachukua pikipiki ambayo ilimpeleka upande mwingine wa kisiwa kile hapo akakuta boti nyingi zinazoenda kwenye visiwa vingine tofauti akapendezwa na kisiwa cha ukala

alichokifanya ni kupanda boti linaloelekea kwenye hiko kisiwa kingine

risaa moja baadaye boti ile ilisimama kwenye kisiwa cha ukala hapa eric akaachia tabasamu la aina yake japo familia yake ilikuwa imehangamizwa hakutaka kujihusisha na mauaji tena hakutaka kuishi kwa visasi ndio maana akaamua kwenda kuishi mbali sana na uso wa Tanzania

baada ya kutoka pale akachukua bodaboda na kuagizwa kupelekwa kwenye nyumba za kulala wageni ambazo zilikuwa nje kidogo ya mji ule

kwakuwa muendesha chombo kile alikuwa mwenyeji wa mji ule hakutaka kupoteza mda akawasha pikipiki na kuitia mafuta kisha wakaondoka mahala pale

safari yao ikaishia kwenye guest ambayo haikuwa na sifa ya kuitwa guest ila kwakuwa kulikuwa na baadhi ya mashuka yakiwa nje aliamini ni guest alichokifanya ni kumlipa yule bodaboda kisha akazama ndani huku akiwa amevaa kofia lake kubwa

chumba chilingi ngapi"aliuliza eric baada ya salamu

elf moja miatano show time na kulala elf tatu"aliongea muhudumu yule

bhasi nitakaa hapa kwa muda wa wiki moja aliongea eric kisha akatoa elf ishirini na tano na kumpa dada yule ambaye baada ya kupokea pesa zile akachukua fungua na kuanza kuelekea kwenye chumba ambacho alitakiwa kumkabidhi eric

baada ya kufika kwenye hiko chumba yule dada akafungua kisha akapiga hatua hadi kwenye kitanda akatoa mashuka na kuondoka nayo na dakika chache baadaye akarudi akiwa na mashuka mengine eric alisimama mlangoni akimuangalia

baada ya kuja na mashuka akayaweka juu ya kitanda kisha akatoka huku akimkabidhi eric funguo

baada ya eric kukabidhiwa chumba akaingia ndani na kuvua begi lake kisha akalitupa juu ya kitanda kile akavua viatu na kwenda kujibwaga juu ya kile kitanda usingizi ukampitia

tumeiua familia yako bado wewe kukuangamiza nadhani utakimbia kote lakini tutakukamata tu hauwezi kukimbiza na pesa ahaa haaa"eric alistuka kutoka kwenye ile ndogo na alipotuliza akili alitambua mlango wake ulikuwa ukigongwa akajinyanyua kiuvivu na kuelekea kwenye mlango ule

akaufungua kuangalia mgongaji wa mlango ule ,aliofungua akakutana na yule dada

naona umelala kwa mda mrefu sana pole na uchovu"aliongea yule dada huku akileta aibuaibu zake za kikekike

kawaida nikusaidie nini"aliongea eric huku akimwangalia yule dada

kuna mama anapitisha chakula kwenye nyumba za wageni sijui unahitaji"aliongea dada yule huku akijiumauma vidole

hapana"aliongea eric kisha akafunga mlango

akaeleka kitandani kwake kisha akalifungua begi lake akatoa picha ndogo akaibusu kisha na kuanza kuiangalia huku moyo ukimuuma sana juu ya familia yake


picha iliyokuwa mbele yake ilizidi kumuumiza eric roho ilimuuma vibaya mno ,hadi anapitiwa na usingizi mawazo juu ya familia yake yalizidi kumzonga

siku hiyo hakutoka nje alikaa ndani hadi mwanga wa siku ya pili ulipochomoza akajiinua kitandani kisha akalisogerea dirisha akachungulia nje huku uso wake ukijikunja kukalibisha kupiga mhayo

akalifata begi lake na kutoa mswaki kisha akachukua na dawa sabuni yake mkononi kuelekea bafubi huko akafanya kila aina ya usafi alioutaka kisha akatika na kuelekea chumbani kwake

akatupa macho kwenye saa yake ya mkanda iliyokuwa mezani akatambua ilishatimu saa mbili za asubuhi akiwa amesimama vilevile akaona tumbo lake jepesi sana hapa akakumbuka alilala bila kula

akatola hadi pale mapokezi huku sura yake ikiwa imejifichaficha kwa kofia kubwa la mzura alilokuwa amevaa akamsalimu yule dada wa mapokezi kisha akauliza sehemu ya kupata sitafutahi

siku zilizidi kupunguza ule mwaka huku ukaribu wa yule muhudumu ukizidi kukua sasa ilipita miezi sita tangu eric awe kwenye kile kisiwa

ilipofikia mwezi wa saba mapenzi kati ya eric na yule dada muhudumu aliyejitambulisha kwa jina la hawa yalizidi kukua mda huo eric alikuwa ameshahamia kwenye chumba anachokaa dada huyo na kazi kubwa aliyokuwa anaifanya ni ya uvuvi

uwezo wake wa kuzama ndani ya maji kutega mitego ya samaki kwa mda mrefu akajikuta akiitwa mzamiaji nani hakuwa akimfahamu mzamiaji hata mtoto mdogo alimfahamu

siku zilizidi kwenda hatimae mwaka ukaisha mala mwaka wa pili ,mwaka wa tatu ukaingia na kuisha mda huo mzamiaji akiwa amejenga kajumba kadogo mahala pale

mwaka wa tatu ukaisha na kuingia wa nne
eric alizidi kufahamika katika kisiwa kile akaamua kufuga midevu ili asitambulike kwa urahisi

huyu mtu yupo ukala mimi nimemuona kwa macho yangu"alisikika bwana mmoja akipiga simu sehemu aliyokuwa anaijua yeye

unauhakika na hilo"ilisikika sauti upande wa pili ikiongea kwa kusisitiza

ni yeye mkuu"alikazia yule bwana na baada ya hapo simu

TSA section A GN
kikao cha siri kiliitishwa katika ofisi hii kubwa ya wapelelezi lilyan akiwa mmoja wa wapelelezi waliokuwa kwenye kikao hiki cha siri

ameonekana huku ukelewe hivyo andaa timu muende kumakamata"alisikika bwana adam akitoa maelezo

sawa mjuu kazi itafanyika"aliongea lily kwa ukakamavu

kikao chao kilichukua dakika 30 mpaka kikaisha mda huo walipanga kikosi cha kwenda kumkamata eric huko ukala

asubuhi ya saa kumi na mbili ndege ndogo aina ya hk 54652 iliyobeba askali 15 ikapasua anga kuelekea mwanza dakika 45 baadaye ndege ile ikatua mwanza mjini hawakutaka kukaa pale wakakodi ndege nyingine iliyowafikisha hadi ukelewe kisha wakapanda gari kuelekea upande wa pili wa kisiwa hapa wakakuta boti ikawavusha hadi ukala wakafikia kweny hotel ambayo isingekuwa laisi kwa watu kuwafahamu

eric hakuwa akijua chochote juu yake hakuwa akijua kama yupo mashakani ilipotimu saa nne kasoro usiku akamuaga mke wake na anaelekea ziwani hakuishia hapo akapiga magoti na kubusu tumbo la mchumba wake kwani tayari alishakuwa na mimba ya miezi mitano baada ya hapo akabeba wavu wake na kuondoka

kikundi maalumu kikajiweka sawa uskiku huu kikao chao kidogo kilikuwa juu ya kumkamata huyu mtu hatari

baada ya kuweka mipango yao sawa wakatoka na kuingia kwenye gari kisha wakaanza safari yakuelekea aliokuwa anakaa eric vijiji vya mbele

baada ya kukalibia kijiji ambacho eric alikuwa anakaa wakashuka kwenye gari na kuanza kunyata kuelekea kwenye nyumba aliyokuwa anakaa eric huku yule mpelelezi akiwaelekeza jinsi ya kuifikia nyumba ile

dakika chache baadaye wakawa wameizunguka nyumba ile Tsa 12 na Tsa 4 wakaishika mitutu yao na kuanza kunyata kuingia ndani ya nyumba ile

jesus ?alisikika Tsa 12 akiongea na kuwaita wenzie washuhudie alichokiona

mwili wa mke wa eric ulikuwa umekatwakatwa vibaya mno huku sehemu yake ya tumboni ikiwa imechanwa na mtoto aliyekuwa tumboni akawa ananing'ia kama anataka kudondoka

huyu si mtu wa kawaida si mmeona alivyofanya mauaji sasa tuwe makini juu ya huyu mtu"alisikika lily akiongea kwa machungu

walichokifanya ni kuweka maaskali watati kwenye nyumba ile kisha wao wakaelekea ziwani kwa bahati nzuri wakakutana na wavuvi ambao bado hawakuingiza mitumbwi yao

yule mpelelezi wa kwanza akaanza kuongea nao kikala kisha yule mpelelezi akaondoka akelekea kule walipojificha wenzao akawap taarifa kuwa eric alikuwa ziwani wakatambua anataka kutoroka walichokifanya wakazileta boat zao za upepo wakazijaza kisha wakaziwekea injini na kuingia ziwani kuanza msako mara moja

eric alikuwa bize na kutega mitego yake akiwa katika hali ya kutokujua mala akaona mwanga mkali ukimmulika kisha amli nzito ikamwambia asifanye chochote akiwa ameduwaa asijue la kufanya akashuhudia maskali wawili wakitoka kwenye ile boti na kuja kwake huku mikononi wakiwa na mitutu

hofu ikampanda hakujua hawawatu wanania gani kwake hapo akafanya jambo ambalo hata wale maaskali hawakuamini


maaskali watatu walishika mitutu yao imara hawakuwa na chembe ya kudhubaa hata kidogo hivyo chochote ambacho eric angefanya bhasi angezawadiwa risasi ambazo zisingekuwa na idadi
na mwishowe kifo

mr eric "ilisikika sauti nyororo ikitokea nyuma ya wale maaskali watatu ,eric aliitambua sauti ile ilikuwa ni ya lily huyu alishawai kuwa naye kwenye mafunzo ya TSA huko nchini cuba miaka mitano nyuma

baada ya lily kuongea vile akawa anakusogea kule eric alipokuwepo mala wimbi zito likatokea wimbi lile likaenda kupiga nyuma ya boti ambayo lili alisimama kutokana na kushindwa kuhimili wimbi lile akajikuta akipelekwa mbele na kuwapiga vikumbo wale maaskali watatu walioshika mitutu

kikumbo kile kikawanyima umakini na kujikuta wakiyumba nafasi hii eric alikuwa akiisubilia kwa hamu kubwa sana kama vile alikuwa akiitegemea alichokifanya alijilusha na kuzama ndani ya maji kisha akaanza kuogelea chini kwa chini kuelekea ufukweni

baada ya wale maaskali wa Tsa kupata umakini tayari eric hakuwapo kwenye ile boti haraka haraka wakawasha taa kubwa na kuanza kumulika ndani ya maji yale

eric alizidi kuogelea kwa kasi hadi akafika nje ya ziwa alichokifanya ni kuanza kueleka kwake kumchukua mke na kutimka mahala pale

alitembe kwa kujificha hadi akafika kwake lakini utulivu uliokuwa nyumbani kwake ulileta hisia ya mashaka kichwani mwake hivyo alichokifanya ni kuzunguka nyuma ya nyuma kisha akapitia kwenye dirisha na kuzama ndani

mawazo yake yalikuwa ni kuelekea chumbani kwa mke wake lakini alipokalibia kwenye chumba chake alijikuta akiteleza na kujibamiza chini kishindo chake kikawafikia wale TSA watatu waliokuwa kwake nao wakaanza kunyata kuelekea ndani

akanyanyuka haraka haraka na kuangalia kilichomtelesha hadi akadondoka vibaya vile

mungu wangu wamemuua"alijisemea eric baada ya macho yake kutua kwenye mwili mfu wa mke wake hasira zikampanda pale alipoona mke wake amekufa kifo kibaya sana kifo cha kudalaluliwa tumbo hadi mtoto aliyetumboni kuning'inia nje

akiwa ameduwaa mahala pale mala akasikia vishindovya watu wakija ndani, akaona mda wowote anaweza kutiwa nguvuni alichokifanya ni kuingia chumbani kwake kisha akachukua begi lake dogo lisilopitisha maji akalivaa kisha akaendea dirisha akapanda na kuruka kwa ne kisha akaanza kutimua mbio vichakani

kishindo chake cha kutua chini kikawasitua wale TSa wakaelekea upande wa nyuma ambao kishindo kile kilisikika

walipofika kule wakashuhudia mtu akitokomea gizani nao hawakutaka kupoteza mda wakaweka siraha zao vizuri mikononi na kuanza kumkimbiza

japo kulikuwa na mwanga hafifu wa mbala mwezi lakini alijitahidi kukimbia huku risasi zikisikika zikimkosa mala kwa mala

wale waliokuwa kwenye boti walipata taarifa kuwa eric anakimbilia upande wa magharibi mwa kisiwa nao hawakutaka kuradha damu wakatekenya injini ya boti ile na ilipocheka wakaelekea upande ambao walielekezwa kuwa eric alikuwa anakimbilia

mbio zake ziliishia kwenye ziwa hapo akakuta mtumbwi ukiwa pambeni akausukumiza haraka haraka majini kisha kapanda akiwa na kuanza kupiga kasia kwa kasi sana

dakika chache baadaye wale maaskali wakawa wamefika mahala pale wakaanza kulusha risasi mfululizo kule ziwani na kwa bahati mbaya moja ikampata mkononi maumivu makali yakaambatana naye ukiachilia mbali damu zilizoanza kumvuja

mawimbi yaliyokuwa ple ziwani yalizidi kumpeleka puta hakuwa na uwezo wa kupambana nayo zaidi alikuwa akihangaika tu huku na kule

akiwa katika hali ya kuhangaika huku mkono ukiwa unamuuma sana kutokana na lile jeraha la risasi kwa mbali aliiona ile boti ikija tena kwa kasi sana

akajinyanyua mahala pale alipokuwa amejiegemeza akashika kamba kwa mkono mmoja kisha akafyatua kamba iliyoshikilia shuka la ngalawa ile

shuka lile likashuka na kukaa sawa kisha upepo mkali uliokuwa ukivuma ukaanza kusukumiza boti yake kwa fujo sana

mwendo ambao alikuwa nao ulikuwa mala mbili ya boti ile ya injini spidi yake haikuwa ya kawida sana

akiwa amewaacha mbali wale mapolisi wa TSA eric akafungua begi lake kisha akatoa kisu kidogo akakifungua kwa nyuma kisha akachukua unga mweusi uliokuwa mahala hapo kisha akawasha kibiriti cha gesi na kukielekeza mahala pale palipopigwa risasi

maumivu makali aliyoyapata yalikuwa hayaelezeki kichwa chake kikaanza kumuuma kwa kasi ya ajabu huku kizunguzungu nacho kikianza kumteka kwa kasi ya ajabu

japo upepo ulikuwa mkali kwenye lile boti lake lakini joto kali likaanza kumpanda kila alipogeuka nyuma alishuhudia wale maaskali wa TSA wakizidi kumfikia

upepo mkali uliokuwa ziwani siku hiyo ulileta dhoruba kubwa sana kwenye boti ya eric hata wale TSA nao walikuwa kwenye wakati mgumu

hali ya eric ilizidi kuwa mbaya ziadi nguvu zilianza kumuisha huku maumivu yakizidi kumuweka sehemu mbaya ,taswira aliyokuwa anaiona mwanzo sasa ikaanza kupotea na dakika chache baadaye akapoteza fahamu


ITAENDELEA

No comments:

Post a Comment